Cheka kidogo

GAY TERRORIST


CHEKA KIDOGO!

A Saudi being interviewed at the US Embassy.

Consul: "Your name please?"
Saudi: "Abdul-Aziz."
Consul: "Sex?"
Saudi: "Six times a week."
Consul: "I mean, male or female?"
Saudi: "Both male and female sometimes even camels."
Consul: "Holy cow!"
Saudi: "Yes, cows & dogs too."
Consul: "Man, isn't that hostile?"
Saudi: "Horse style, dog style, any style!"
Consul: "Oh dear!"
Saudi: "Deer? No deer, they run too fast...!"

THE KENYA POLICE


KAMANDE PETER KINYANJUI

PAYSLIP


MONTH: JUNE 2007


Basic Salary 15,000

Hse allowance 0

Gross salary 15, 0000


Deductions


Magereza SACCO 3000.00


NHIF 320.00


NSSF 200.00


PAYE 2740.00


Loan repayment 3260.00


KCB LOAN 2250.00


Total Deductions 11770.00


Net Pay 3230.00

BREAKING NEWZZZZZZZ......

BILIONEA CHENGE AJIUZULU

KWAHERI DITTO

Pichani ni Mwili aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri ukipakiwa katika gari tayari kupelekwa katika chumba cha kuifadhia maiti cha hospitali ya mkoa wa Morogoro mchana huu mara baada ya kufariki dunia ghafla kwenye Hotel ya Hilux mjini Morogoro.Kifo chake kimethibitishwa na mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa, Dk. Meshack Mmasi ambaye amesema alimpokea marehemu akiwa ameshafariki.

bongo tambarale

MWANANYAMALA IONEKANAVYO LEO ASUBUHI BAADA YA MVUA ZA JANA USIKU.





najua mnajua ila hii ni muhimu kujua zaidi

HABARI ZA KUTHIBITIKA!

Ufisadi WA Samwel Sitta

Ama kweli, ukistaajabu ya Mussa, utayaona ya Firauni!
Kama unadhani vigogo wa EPA ni mafisadi peke yao ,
basi ulikuwa hujamfahamu Spika wa Bunge SAMUEL JOHN
TEGEZA SITTA ! Ukimsikiliza anapoongea unaweza kuamini
kwamba kiongozi huyo wa Bunge ni msafi kutokana na
umahiri wake wa kujivalisha sifa kemkem – Mr Misifa.

Unakumbuka hivi karibuni alivyomtukana Naibu Spika eti
hawezi kusimamia mambo nyeti mpaka awepo yeye mwenye
Bunge? ! Kisa nini? Kupenda sifa na kumdhalilisha
mwenzake mbele ya umma, halafu bado anaendelea kuliita
Bunge eti ni chombo cha kidemokrasia!

Tumebaini kwamba Sitta amekuwa akijimiminia sifa
nyingi ili kulinda ufisadi anaoufanya usigundulike
katika jamii yetu. Ngoja nikupe tone tu la madhambi
yake kwa umma ili uone ni hatua gani utachukua, na ili
na yeye ajipime kwa nafasi yake. Angalia uchafu huu:--


Anatumia vibaya fedha za umma. Amekuwa akitumia
msaidizi wake kuchota mapesa kwa kisingizio kuwa ni
masurufu ya safari za ndani na nje ya nchi. Kila
safari ya siku moja ndani ya nchi huchukua shilingi
Milioni tano (5,000,000/=), na kila safari ya siku
moja nje ya nchi huchukua shilingi Milioni Kumi na
Tano
(15,000,0000/=).

Ameshindwa kufanya marejesho ya masurufu (imprest)
hayo, licha ya kupeleka risiti kadhaa za kughushi/za
uongo kwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Bunge. Mpaka sasa
anadaiwa jumla ya shilingi Milioni sitini
(60,000,000/=) za masurufu.-

SITTA hupeleka risiti za uongo kwa Mhasibu Mkuu,
zikionesha madai kutoka Oysterbay Pharmacy ya Shilingi
Milioni Mbili (2,000,000/=) aliyotumia kwa tiba kila
wiki.- Amekuwa akilazimisha hawara yake wa Hospitali
ya Aga Khan naye alipwe posho kama wabunge anapokwenda
naye Dodoma. Kwa mfano, hawara huyo alilipwa 'per
diem' kuanzia tarehe 13/12/2007 hadi tarehe 31/01/2008
(Siku 50). Huo ni Ufisadi mkubwa!

Anaye kimada wake mwingine anayekwenda kwa jina la
ASIA ambaye anaishi nyumba Na. 111 karibu na
Mahakama ya Ardhi Upanga na amezaa naye. Huko mtaani
kwao kimada huyo hujiita mama SITTA, na ni dada yake
aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa iliyokuwa Tume ya
Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC). Mwanamke huyo
muda wote hutumia gari la Ofisi ya Bunge STK 232
Toyota RAV 4.

Pia anaye kimada mwingine (jina limehifadhiwa) ambaye
anaishi kinondoni (Livingstone), mtaa wa Honolulu
katika nyumba ya kupanga nayomilikiwa na dada yake
Kawawa. Nyumba hiyo inatazamana na Nyumba Na.
KH.MK/No. 337 katika mtaa huo huo. Kimada huyo hutumia
gari ya kiofisi ya Spika mwenyewe STK 3002.- Vimada
wote hao hupata huduma za maji na umeme kwa gharama za
Ofisi ya Bunge.

Kuna kipindi mke halali wa Spika, aliwahi kulalamikia
hali hiyo. Kuna siku maji yalikatika nyumbani, mke wa
Spika akaomba apelekewe ' bowser' la maji na Ofisi ya
Bunge. Ohooo! Watekelezaji wakapeleka maji kimakosa
kwa kimada. Mama Sitta akashtukia dili.

Kuna taarifa kwamba mnamo Mwezi Oktoba 2007, Kamati ya
Bunge ya Hesabu za Serikali PAC) iligundua mapungufu
makubwa katika matumizi ya fedha yaliyofanywa na Spika
SITTA. nimedokezwa kuwa Spika aliwanyamazisha wajumbe
wa kamati hiyo, ambapo aliwatishia kutowapatia posho
na safari za nje kama wangeyafumua mapungufu yake
hadharani! Hapo inaonesha kuwa wajumbe hao walipewa
rushwa!!

Kama JK anataka viongozi wa kisiasa na wa serikali
watenganishe biashara na uongozi wa ku – 'sacrifice'
kimojawapo, hilo litakuwa gumu kwa sababu Sitta
alipokuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha cha
Uwekezaji nchini (TIC) alitumia nafasi hiyo kuingia
ubia na wafanyabiashara wengi wa Kigeni. Je, Wizara
ya Maliasili na Utalii inatambua kuwa Spika ana hisa
kwenye kampuni moja ya Kichina inayosafirisha nagogo
licha ya marufuku yaliyowekwa?!

Nililokupa hapo ni tone tu.

chenge atua bongo kujibu mapigo

Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge akijibu mwasali ya waandishi wa habari juu ya shutma za kujilimbikizia fedha muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam jana mchana akitokea nchini China katika alikokuwa ziarani na Rais jakaya Kikwete

BBC Kusaka wafanyabiashara vijana


BBC inatafuta vijana wenye mawazo ya kibiashara kushiriki katika shindano lijulikanalo kama Faidika na BBC, litakalozinduliwa rasmi Jumatatu Aprili 21 2008.

Faidika na BBC inaalika vijana wanaozungumza Kiswahili, na wenye umri wa kati ya miaka 16 hadi 24, kuwasilisha michanganuo yao, ya jinsi ya kuanzisha biashara ambayo itanufaisha jamii. Mchanganuo huo utatakiwa kuwiana na bajeti ya Dola za Marekani 5,000, zitakazotolewa, ikiwa ni zawadi ya kwanza na kuwa msingi wa biashara hiyo. Mchanganuo usizidi maneno 1,500. Michanganuo itumwe kwa: faidika na BBC, PPF Building, 8th Floor, P.O Box 79545, Dar es Salaam. Au kwa barua pepe: faidika@bbc.co.uk.

Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Solomon Mugera, amesema "Shindano hili ni fursa kwa vijana wenye kuona mbali, na ni nafasi yao ya kutimiza ndoto zao. Hii pia ni nafasi kwa vijana kujisaidia wao wenyewe na jamii zao kwa ujumla".

Salim Kikeke, Meneja Mradi wa Faidika na BBC ameongeza "Nina imani kuwa vijana wengi wana mawazo mazuri na ya kuvutia ya kibiashara. Kwa wale ambao hawatashinda zawadi ya kwanza, tutajitahidi kuwatafutia ushauri wa kuwasaidia katika kutimiza ndoto zao".

Kutakuwa na mchuano wa kutafuta mshindi mmoja kutoka kila nchi. Kuna jumla ya nchi sita zinazoshiriki katika shindano hili. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda, na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. Mchuano wa kutafuta mshindi wa Rwanda na DRC utafanyika kwa siku moja. Mchuano wa Tanzania utafanyika Jumatano tarehe 4 mwezi Juni. Mshindi kutoka nchi husika atazawadiwa cheti maalum na kombe.

Washindi sita, mmoja kutoka kila nchi zilizoshiriki, watapambana kuwania nafasi ya kwanza mjini Kampala, Uganda, Jumatano, tarehe 18 Juni. Fainali hiyo itatangazwa moja kwa moja kupitia matangazo ya jioni ya BBC, Dira ya Dunia, na vilevile katika mtandao kupitia bbcswahili.com. Mshindi atapata dola elfu tano za Marekani, pamoja na Kombe. Jopo la majaji litaundwa na wafanyabiashara vijana kutoka Afrika Mashariki na Kati.

David Ssegawa, kijana mwenye umri wa miaka 22, raia wa Uganda, alikuwa mshindi wa Faidika na BBC mwaka jana baada ya kuwashinda washiriki wengine zaidi ya 5,000, kutoka eneo la Afrika Mashariki na kati, wanaozungumza Kiswahili. David aliandika mchanganuo wa utengenezaji mishumaa. Hivi sasa amekwisha anza biashara yake na inaendelea vizuri. Kupata habari zaidi kuhusu David Ssegawa, pamoja na shidano la Faidika na BBC ingia katika mtandao wetu bbcswahili.com.

smallest girl





Tiny teenager from India is smallest girl in the world



Last updated at 14:13pm on 7th April 2008

A teenager from India who stands at a tiny 1ft 11in (58cm) tall is the smallest girl in the world.

Jyoti Amge, 14, is shorter than the average two-year-old child and only weighs 11lb (5kg).


Cheka kidogo

ANGALIA MZUNGUKO WA SAA YAKO.

Kuna mtu mmoja alifariki dunia na akaenda kwa Mungu,alipofika akakuta saa za ukutani nyingi sana zimetundikwa. Akauliza 'Hivi hizi saa ni za nini huku?' Akajibiwa na Askofu mkuu aliyemkuta huko, 'Kila saa ina dhambi za kila Binadamu,ikizunguka mara moja ina maana ametenda dhambi mara moja'.

Yule jamaa akauliza 'mbona hii hapa imesimama ni mbovu? Akaambiwa hiyo ni ya mama Theresa, na inamaanisha kuwa hakutenda dhambi kabisa ndio maana imesimama.

Jamaa ikabidi aulize tena, 'hivi saa ya Edward Lowasa na Ballali iko wapi kati ya hizi?' akajibiwa, 'ya hao ndugu iko ofisini kwa Bwana Yesu mwenyewe maana anaitumia kama feni kwa jinsi inavyozunguka mara nyingi na kwa kasi.'

Bongo tambarale

hapa ni mitaa ya upanga kama inavyoonekana jana jioni baada ya mvua


JOKETI mrembo mwenye vipaji lukuki



KAMA umfuatiliaji najua hii ushaishtukia; Jokate Mwegelo Balozi wa Redds 2006, aliyekuwa pia balozi wa gazeti bora kabisa la kiingereza nchini linalochapishwa na kampuni ya Mwananchi Communications, The Citizen ambaye pia alitwaa taji la Miss Tanzania namba 2 ni miongoni mwa vijana wa kitanzania wenye vipaji lukuki na mashaallah anavitumia ipasavyo.

Utakumbuka kuwa kabla ya Jokate kutwaa mataji hayo, cheche zake zilianza kuonekana mara tu alipojitosa katika kinyang�anyiro cha kumsaka Miss Kurasini na hatimaye alitwaa taji la Miss Temeke.

Maiti iliyogombewa Dar yazikwa

HATIMAYE mwili wa marehemu Paul Goliama (40) umezikwa na ndugu zake ambao ni waumini wa dini ya Kikristo badala ya waumini wa Kiislamu katika makaburi ya Sinza, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Mwananchi jana, Shemeji wa marehemu, Ibrahim Msumari, alisema mazishi ya marehemu Goliama yalifanyika jana majira ya saa 8:00 mchana katika makaburi ya Sinza, jijini Dar es Salaam kwa amani na utulivu.

Msumari alisema baada ya kutoka katika eneo la mazishi, watu wote walielekea nyumbani kwa marehemu walipoweka matanga ili kuungana na ndugu jamaa na marafiki wa familia ya marehemu.

Machi 28, ulizuka mzozo mkubwa wa kugombea maiti hiyo baina ya waumini wa dini hizo huku kila upande ukidai kuwa ndiye mwenye haki ya kuizika maiti hiyo.

Mzozo wa huo ulidumu kwa zaidi ya saa tano katika Kanisa la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Jimbo la Kinondoni Usharika wa Sinza muda mfupi baada ya mwili wa marehemu kupelekwa kanisani hapo kuombewa sala za mwisho kabla ya mazishi.

Baada ya jitihata na busara za Mchungaji wa Kanisa hilo, Tuheri Tuheri pamoja na Imamu wa Msikiti wa Safwa za kujaribu kusuluhisha mzozo huo zilishindikana, Jeshi la Polisi iliamua kuuchukua mwili huo na kuurudisha katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam mpaka mahakama itakapotoa maamuzi kuhusu dini ambayo ilistahili kumzika marehemu.

Machi 31, ndugu wa marehemu waliamua kwenda kufungua kesi katika Mahaka ya Kinondoni kudai kuuzika mwili huo ambapo juzi mahakama ilitoa uamuzi kuwa mwili huo uzikwe na ndugu zake.

Sababu kubwa iliyosababisha ya mwili huo kugombewa na dini mbili ni kutokana na marehemu kubadili dini mwaka 2004 kutoka Ukristo kwenda Uislamu na hatimaye mwaka 2006 akabadili tena toka Uslamu kurudi Ukristo.

Utapeli wa aina mpya Dar

*Matapeli wajifanya waganga wa jadi
*Mwanajeshi mstaafu ajikuta akiuza nyumba, gari
* Alirubuniwa anatafutiwa tiba ya tumbo

UTAPELI wa aina yake umeibuka jijini Dar es Salaam na kusababisha watu mbalimbali kujikuta wakipoteza mali zao katika mikono ya matapeli wanaosadikiwa kutumia nguvu za giza kuwarubuni watu.

Katika sakata la hivi karibuni, mzee aliyefahamika kwa jina la Said Makau, mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), amejikuta akiuza mali zake zote ikiwamo nyumba, gari na vitu vya ndani vyenye thamani ya zaidi ya Sh 71.5 milioni bila kujijua.

Tukio hilo lilitokea katika eneo la Bonyokwa Vyumba Vinane jijini hapa baada ya Makau kudaiwa kuwa alikuwa akidanganywa na matapeli kwa kunyweshwa dawa za kienyeji ili kumzubaisha akili.

Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwake, Makau, alisema watu hao walimwandama kwa takriban mwaka mzima ambapo awali yeye na familia yake walikuwa wakiishi katika eneo la Tandale kabla ya kuhamia katika nyumba yao, Septemba mwaka juzi katika eneo hilo la Kimara.

Alisema mara nyingi amekuwa akisumbuliwa na tumbo la kujaa gesi, jambo lililomfanya ahangaike katika hospitali nyingi bila mafanikio na ndipo alipokutana na kijana mmoja (jina linahifadhiwa) ambaye ni fundi simu.

Alisema baada ya kumhadithia kijana huyo matatizo yake, alikubali kumsaidia kwa kumwambia kuwa yanaweza kutatuliwa na waganga wa jadi ambao anawajua.

Mwanajeshi huyo mstaafu, alisema kijana huyo tangu hapo amekuwa karibu na familia yake na kwamba baadaye hakuweza hata kushtuka kuwa anaweza kumgeuka.

Alisema siku ya siku bila kujua kuwa anatumbukizwa katika dimbwi la kitapeli, alikubaliana na kijana huyo kwenda kwa mganga eneo la Kibangu na kuwakuta vijana wengine ambao walijitambulisha kuwa ndio waganga wa jadi.

Alisema watu hao walimweleza kuwa ni kweli ana matatizo makubwa kwani nyota yake imechafuka na kama hatapatiwa dawa kwa haraka angeweza kupoteza maisha yake kwa kifo cha ajali na familia yake yote ingeteketea.

Kwa mujibu wa Makau, walimpatia dawa za kunywa zilizowekwa katika glasi ya maji na hirizi ambazo alidai ndizo zilisababisha kuchanganyikiwa na kuwa katika hali ya kupoteza kumbukumbu, kisha kukubali kufanya kila jambo analoamrishwa bila kukataa ama kujua kama ni baya ama zuri.

Alisema kabla ya kunywa dawa hiyo, waganga hao walimpa masharti atumie peke yake bila kumshirikisha mkewe na kumuonya akimwambia mtu atakufa pamoja na watoto wake wote.

Alisema siku zilizofuata kijana huyo akiwa na mwenzake walimfuata nyumbani kwake na kumweleza kuwa, anatakiwa kutoa kadi za gari na gari lake aina ya Hiace alilokuwa akilitumia kama daladala kwa safari za Ubungo- Segerea ili litambikiwe kwa mizimu.

Akielezea jinsi utapeli ulivyofanyika, mzee huyo, alisema matapeli hao walimfuata na kumwambia kuwa kama hatalipeleka gari lake kwenye mizimu kuombewa litaweza kuua watu wengi ndani ya wiki moja; na kumsababishia matatizo makubwa kwa askari wa kikosi cha usalama barabarani na kutiwa hatiani.

Ili kuendelea kudumisha miiko ya waganga wale, alisema ilimlazimu kumdanganya mkewe na watoto wake kuwa gari linapelekwa kutengenezwa.

Alisema walimwelekeza kulipeleka gari hilo na kadi zake katika maeneo ya Manzese kwenye ofisi iliyoko uchochoro wa Moshi Hotel na kuwakabidhi.

Makau anasimulia kuwa, alipowakabidhi, walilizunguka gari hilo kana kwamba wanaliagua kisha kumwambia inabidi liuzwe ili anunuliwe jingine kulingana na mizimu ilivyoamua.

"Niliposita watu wale waliniambia basi itabidi niliache gari langu pale ili waendelee kuliagua na wakaniomba nirudi kulifuata baada ya wiki moja kazi ya maombezi itakuwa imekamilika," alisema.

Katika kumwondoa hofu, alisema watu wale walimwambia asaini kwenye mkataba wa makabidhiano, ili akija kulichukua kusiwe na hadithi yoyote.

Kwa kuhofia madhara yanayoweza kutokea kwa kusababishwa na gari hilo, alikubali kuliacha gari hilo huku akiwa hana majibu kwa nini alikubali kufanya hivyo.

Baada ya wiki kupita, alikwenda kwenye ofisi ile kuchukua gari lake, lakini alistaajabu baada ya kukuta haipo wala watu hawapo. " Nilipoona sielewi niliamua kuuliza baadhi ya watu maeneo yale ambao hawakuwa wakinielewa natafuta nini," alisema.

Aliamua kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa na kupewa RB kwa ajili ya kuwakamata watuhumiwa hao.

�Njiani nikakutana na yule bwana aliyejifanya kama karani siku ile nikamsimamisha nikataka kumuuliza inakuaje, aliponiona alikimbia mbio na kuniacha nikiwa na butwaa,� alisema.

Alisema alipoona siku zinakwenda aliamua kumtafuta yule kijana ili amweleze kuwa watu wake wamemtapeli, akamtuliza asiwe na wasiwasi kwa kuwa gari wameliuza na watamnunulia jingine.

"Walipoona kuna dalili za njama zao kujulikana waliniletea dawa nyingine na kumshauri kutumia tena, ila safari hii ampe na mke wake na nyingine wapigie deki nyumba yote ili apone haraka na waendelee kutunza siri yao," alisema

Makau, alisema dawa hizo ziliendelea kumchanganya na mkewe, na kwamba kwa safari hiyo, walikuwa na mkakati wa kumtapeli nyumba na kuchukua vitu vyote vya ndani vyenye thamani ya Sh 1.5 milioni kwa madai kuwa wanaenda kuvipooza kwa mdawa.

Alisema walipovichukua vitu hivyo walienda kuviuza kwa Sh 450,000 kisha kurudi kumchukua yeye na kumpeleka katika makaburi ya Ismailia yaliyopo Makumbusho, ambako walimsomea dua kwa saa mbili wakidai kuwa angepata nafuu.

Alisema katika hali isiyo ya kawaida, siku tatu zilipopita tangu wachukue samani hizo, walirudi tena nyumbani kwake na kudai kuwa nyumba wanayoishi ina majini mengi, hivyo ni vema wakaiuza na kununua nyingine, kabla hayajaanza kuwadhuru.

Baadaye kijana huyo akiwa na mtendaji serikali za mitaa, Athuman Mtono, walifika nyumbani kwake na kumweleza kuwa anatakiwa kuita mashahidi kwani wateja wa kununua nyumba tayari wamefika.

Alilazimishwa kusaini fomu iliyoandikwa hati ya uthibitisho wa kiwanja badala ya hati ya mauzo ya nyumba bila kujijua kuwa ndiyo anauza nyumba kwa mnunuzi kwa gharama ya Sh22 milioni.

Baada ya kusaini hati hiyo, mdogo wake mnunuzi wa nyumba hiyo alitoa Sh 1milioni na kudai fedha nyingine kiasi cha Sh 21 milioni zitapelekwa kesho yake na kwamba ananunua kwa ajili ya kaka yake ambaye hakuwepo siku ya tukio hilo.

Mtono lithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa Makau aliamua kuuza nyumba yake kwa ridhaa yake mwenyewe kwani siku ya tukio alikuwapo mkewe na mtoto wao.

Naye Mjumbe wa Shina, Raphael Fikiri alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa walikabidhiwa fedha kiasi cha Sh20,000 kila mmoja kama mashahidi wa kuuzwa kwa nyumba hiyo.

Fikiri, alisema baada ya tukio la kuuzwa kwa nyumba hiyo, alishuhudia teksi ikifika katika eneo la nyumba na kuondoka na mtuhumiwa.

Makau, alisema waligundua kuwa wametapeliwa wakati mnunuzi alipokwenda kuwatoa katika nyumba yao na ndipo walipochukua hatua ya kwenda kuripoti katika Kituo cha Polisi Mbezi kwa Yusufu na kupewa RB/749/2008 ili watuhumiwa waweze kukamatwa.

Alisema kwa kushirikiana na askari wapelelezi walifanikiwa kumkamata kijana huyo, eneo la Malamba akiwa anasimamia ujenzi wa nyumba yake.

Baada ya kukamatwa wameendelea kufuatilia kesi hiyo maeneo mbalimbali ya usalama, lakini amekuwa akizungushwa, wakati huo huo wanunuzi wa nyumba hiyo wanawashurutisha kuhama kupitia kwa mtendaji.

Alisema hivi sasa wamepewa barua yenye kumbukumbu namba MAA/DL-03/08/11 kutoka kwa wakili wa wanunuzi hao, ambao ni kampuni ya (M&A Advocates ) inayowataarifu kuwa wanatakiwa kuhama, vinginevyo hatua za kisheria zitafuata.

Mwananchi ilifanikiwa kuongea na mpelelezi wa kesi hiyo kutoka katika Kituo cha Polisi cha Mbezi kwa Yusufu ambaye alikiri tukio hilo kuripotiwa kituoni hapo.

Hata hiivyo, alikataa kuzungumzia zaidi kwa madai si mzungumzaji wa Jeshi la Polisi, Mkoa wa Kinondoni bali, mwenye dhamana hiyo ni Kamanda Jamal Rwambo.

Habari za ndani kutoka polisi zinadai kuwa jalada lililokuwa na vielelezo vya kesi hiyo vilibadilishwa ili kuweza kumtetea mtuhumiwa asiweze kukabiliwa na kesi ngumu ya kitapeli dhidi ya Makau.

Inadaiwa kuwa kutokana na ubabaishaji katika kesi hiyo, mpelelezi mkuu wa kanda alimwamuru askari huyo, kupitia upya mwenendo wa kesi hiyo ili mambo yote yaweze kutendeka kwa haki.

Kamanda Rwambo alipohojiwa kwa simu na Mwananchi alisema kuwa ni vema akapewa muda ili aweze kufuatilia jambo hilo, kwani tukio hilo lilipotokea alikuwa yuko likizo, hivyo asingeweza kuongea kitu chochote.

Hata hivyo, katika uchunguzi wa polisi na familia ya Makau, gari hilo limekamatwa na linadaiwa kuuzwa kwa watu wengine wawili na baadhi ya vitu vimerudishwa baada ya Mzee Makau kutumia fedha kuvikomboa kutoka katika mikono ya waliovinunua.

Uingereza yazidisha masharti kwa wageni

UINGEREZA imeongeza masharti ya kupatikanaji wa viza zake na kuweka adhabu ya kifungo cha miaka 10 ya kutoingia nchini humo kwa waombaji wa viza watakaobainika kughushi nyaraka.

Afisa Habari wa Ubalozi wa Uingereza nchini, John Bradshaw jana alisema kuwa, alisema adhabu hiyo itakayotolewa duniani kote, itaanza kutumika kuanzia Aprili mosi mwaka huu.

" Aprili mosi mwaka huu, mtu yeyote ambaye huko nyuma aliwahi kuvunja sheria zetu za uhamiaji na kwenda nchini Uingereza kinyume cha sheria au kutumia udanganyifu katika maombi ya viza atapigwa marufuku kuingia Uingereza kwa kipindi cha kufikia hadi miaka kumi," alisema Bradshaw.

Bradshaw alitaja mambo yanayoweza kumsababishia mtu adhabu hiyo kuwa ni kufanya kazi nchini Uingereza kinyume cha sheria, kuishi siku 28 zaidi ya muda ulioonyeshwa kwenye viza yake, kwenda nchini humo kinyume cha sheria na kughushi nyaraka katika kutuma maombi ya viza.

Alisema nchi hiyo imeamua kutoa adhabu hiyo ili kudhibiti ongezeko la vitendo vya kutumia nyaraka za kughushi kwa waombaji wa viza wanaotaka kwenda Uingereza wanaotumia nyaraka za kughushi nchini.

Alisema katika kipindi cha mwaka 2006/2007 pekee asilimia 17 ya watu 562,556 walioomba viza za Uingereza walinyimwa kutokana sababu mbalimbali ikiwamo kughushi vyeti ambapo nchini Tanzania asilimia ya watu walionyimwa vyeti hivyo ni 16.

Katika hatua nyingine, Ubalozi huo nchini umeanzisha mfumo mpya wa uandaaji na upatikanaji wa viza ambapo kuanzia sasa viza zitapatikana siku ya kazi inayofuata badala ya siku moja kama ilivyo awali.

Bradshaw alisema hilo limesababishwa na uongezeko la uhitaji wa kufanya uchunguzi zaidi kiusalama ambapo sasa uchunguzi huo unafanyika kutoka sehemu moja (Centralised), Uingereza

Cheap Mobile Phone

KT51 Specification

Product Model

KT51

Feature

Ultra low end mobilephone.

Long standby and talking times.

upper slim, supper light

Network operator customization support.

Specification

Appearance

Type

Low end

Style

Bar Phone

Dimensions

103*44*13.7MM

Color

Black, silver

Wheight

60 g

Display

1.5'' FSTN with color film, 96*64

Basic Function

Frequency

GSM 900MHz/1800MHz

speaking time

>200 min

languages

Chinese, English, French, Spanish, Russian, Arabic, Turkish, Vietnamese……

Standby time

>110 hours

Other function

Antenna

Embedded

Address list

No ME phonebook, capability depends on SIM card

SMS

Support, no ME SMS, capability depends on SIM card

chord

16 chord software MIDI

STK

support

Input method

Chinese, English

SMS

support

accessories

550mA Li-batteryand 1 piece of charger

1. Sample Price: USD 27.9 / PC,

MOQ=100 pcs Price: USD 26 / PC

More than 500 pcs Price: USD 25.4 / PC

2. Lead Time for Sample: 3 days after receipt remittance

MOQ=100 pcs, 15 days after the receipt remittance

3. Keep one year warranty


tamko la CUF juu ya muafaka na CCM




Tarehe 17 Machi, 2008, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama Cha Wananchi (CUF) lilifanya kikao chake mjini Zanzibar ambapo lilipokea na kuridhia makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Siku hiyo hiyo, CUF iliwatangazia wanachama wake na Watanzania kwa jumla matokeo ya kikao hicho cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Demokrasia, mjini Zanzibar.

NI Aibu"

The Land of Kilimanjaro, Olduvai, Serengeti, Tanganyika, Zanzibar, Ufisadi and Uchawi!.... of course there are exceptions!
Na ndiyo ukweli wenyewe kwa baadhi ya WaTz.
Wametusema sawasawa.

Nchi ya wachawi?

Na ndiyo maana bado tunabishana kuhusu nani ameficha kiatu cha kukimbilia, wakati wenzetu wameshajipanga kwenye mstari. Na tukishakipata kiatu cha pili tunacholitafuta, kiatu cha kwanza watakuwa wajinga fulani fulani wanaojiona werevu sana wamekificha ama wamekitoboa. Yaani ali munradi tuna visingizio gunia tele.
Kazi tumekalia kusema na kuamini uchawi, uvivu, kusemana, kutafutana visa, kuomba omba na kuamini miujiza tuuuuuu badala ya kufanya kazi kwa bidii, juhudi na maarifa. Yaani mtu anaamini kabisa kuwa atapataga mautajiri ya fasta fasta kwa ulozi. Hata anayejitahidi kufanya kazi anaogopa kutishwa kulogwa. Yaani ni aibu mfanowe hakuna.

Dawa?
Elimu inayoendana na wakati na mazingira. We mtu anafundishwa nadharia tu shuleni, vipindi vya vitendo, maabara hamna vifaa ya kutosha ama hakuna kabisa vifaa, anaishia kukariri tu, sasa huyu mtu akihitimu atatarajiwa vipi afanye kazi kwa ufanisi? Ndiyo usanii tena unakuja bila kutaka. Maneno meeengi, kuagiza kwiiingi, lakini mwambie akuonyeshe kwa mfano kwa vitendo..... utasikia, 'fanya tuu', 'yaani hujui', 'hiyo rahisi', Ningejua ningeuliza? Shule ndiyo zimeshakuwa sehemu za kukulia tu sasa na kujifunza ujamaa! Maanake walimu wanasema utajifunza utapoanza kazi!


Wengine wenu mtanichukia tu lakini ndiyo hivyo tena, nimeshayasema mawazo yangu, kwani nimekulazimisha ukubali? Hatufanani!

hotuba

Hotuba Ya Rais Kwa Taifa

Ndugu Wana-CCM Wenzangu;
Viongozi na Wanachama Jumuiya za CCM;
Ndugu Wananchi;

Kama mjuavyo tumejiwekea utaratibu wa Rais kuzungumza na taifa kila mwisho wa mwezi. Lakini, kwa mwisho wa mwezi wa Machi nilishindwa kufanya hivyo kwa sababu ya kulazimika kwenda Mererani, Mkoani Manyara ambako kumetokea maafa makubwa kwa wachimbaji wa madini.

Maafa hayo yalisababishwa na mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa zilizonyesha katika eneo hilo usiku wa tarehe 28 kuamkia tarehe 29. Nilikwenda kuwafariji wenye migodi, wachimbaji na familia zao kwa maafa yaliyowakuta. Pia nilikwenda kuona shughuli za uokoaji na uopoaji wa miili ya wale waliofariki. Soma zaidi:

http://hakunakulala.blogspot.com

Powered by Blogger